Kampuni inayojishughulisha na utengenezaji na Usambazaji wa Filamu hapa
Tanzania ‘Proin Promotions’ sasa yapiga kambi jiji la Mwanza kwa ajili
ya kusaka vipaji.
Proin Promotions Limited ni kampuni iliyokuja kwa kasi na kupata mafanikio kutoka na kazi wanazozisimamia kuwa na ubora wa juu.
Proin Promotions Limited ni kampuni iliyokuja kwa kasi na kupata mafanikio kutoka na kazi wanazozisimamia kuwa na ubora wa juu.
Kwa sasa kampuni hiyo imekuja na kitu kipya cha kusaka vipaji
inayofahamika kwa jina la ‘Tanzania Movie Talents’ na sasa ipo jijini
Mwanza ikiendelea usakaji wa vipaji vya kuigiza filamu meneja wa masoko
wa Proin Promotions Bw. Evance Stephen aliongea na mwandishi wa
Baabkubwa na kusema.
“Proin Promotions Team tupo tupo Mwanza na tunaendelea na mchakato wa
kumtafuta mshindi wa ili aweze kuungana na wenzake katika mikoa mingine
na mshindi wa kanda ya ziwa anatarajia kupatikanika siku ya kesho,
jumapili na baada ya hapo tutaelekea katika kanda zifuatazo ,kanda ya
kati Dododma, kanda ya kaskazini Arusha, kanda ya juu kusini Mbeya,
kanda ya kusini mashariki Mtwara na special zone Kigoma, na baadae
kuingia kambini Dar es Salaam.” Evance alisema
Chapisha Maoni